JUAKALI

 Juakali Mimi Juakali

Heshima nami utanipa

Chepeo lazima utaivaa

Mwavuli  utanunua 

Kivulini utaketi 

Sababu Mimi ni Juakali.


Juakali Mimi Juakali

Mbona mwanidhulumu mie?

Asubuhi na mapema safarini nipo 

Mchana yote kwenye Juakali 

Jasho natokwa riziki nipate 

Mchafu mie, takataka mwanifananisha.


Juakali Mimi Juakali 

Nisipongaa mngali baridi 

Maganjwa mtayapata 

Lishe na siha njema mtaikosa 

Heshima yangu mtanipa. 


Juakali Mimi Juakali

Mali zangu sharti mwahitaji  

Mbona Hela mwanipuja? 

Wazimu mwanilinganisha 

Tafadhali, mie pia adhamu. 


Mimi Juakali heshima Nampa Juakali 

Asubuhi kabla ya Juakali 

Naraukia Juakali lishe kwa aushi nipate 

Bidhaa zangu naziweka kwa Juakali 

Heshima zangu mupokee wenzangu Juakali


# Milcah the Poetess

@ Kenyan Mind Speak.














JUAKALI JUAKALI Reviewed by Milcah the Poetess on June 25, 2022 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved. Kenyanmindspeak. Powered by Blogger.