HONGERA DADA

Bintiye mwenye heshima ,ee Mungu akubariki

Kitisiti kasimama,wanadamu wahakiki

Walosema utazama,wote sasa ni shabiki

Tabasamu uwapee ,usiwe nao na chuki.

 


Shuleni ulieenda,baba katoka ghafula

Wakanena hutaenda ,bahati kaja ghfula

Mama kasema taenda,wadaku waone bala

Tabasamu uwapee,usiwe nao na chuki

 

Inne miaka kapita ,dato inne kamaliza

Kijiji basi katoka, akili enda tuiza

Gange kaenda tafuta ,zahela hujamaliza

Tabasamu uwapee,usiwe nao na chuki

 

Maadui kakujia ,walidhani tashindwa

Akilini kaamua ,kamwe hutashindua

Riziki jitafutia ,maadui watadua

Tabasamu uwapee,usiwe nao na chuki

 

Maurine lako jina,sijui lake maana

Kweli basi tang'ang'ana, kujua lake maana

Heshima wako maana,baraka kwako kwa pana

Tabasamu uwapee , usiwe nao na chuki

 

Wako mgeni kawasili, jina Darliah ukampa

Kwa shairi taasili,hongera nami takupa

Wambea iwaasili,aibu kweli mewapa

Tabasamu uwapee,usiwe nao na chuki

 

Nina mengi kuwaambia,kwa kifupi takatia

Beti saba malizia,bali sitanyamazia

Hongera dada pokea, kweli we wajishindia

Tabasamu uwapee,usiwee nao na chuki.

HONGERA DADA  HONGERA DADA Reviewed by Milcah the Poetess on December 20, 2020 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved. Kenyanmindspeak. Powered by Blogger.